Monday, April 13, 2015

Wafanyabiashara wa vitunguu Singida walia na Waganda, Wakenya


Singida. Wafanyabiashara wa vitunguu katika Soko la Misuna, Singida wameiomba Serikali kuwasaka na kuwakamata wafanyabiashara kutoka Kenya na Uganda wanaonunua zao hilo moja kwa moja kutoka kwa wakulima kwa madai kuwa wanawanyonya wakulima na kuikosesha halmashauri mapato.

Thursday, January 8, 2015

KILIMO BORA CHA MAHINDI


Tokeo la picha la kilimo cha mahindi
Tokeo la picha la kilimo cha mahindiTokeo la picha la kilimo cha mahindiMahindi ni chakula muhimu na ni aina ya nafaka katika mataifa ya Afrika yaliyomo kusini mwa jangwa la Sahara. Ni chakula cha matumizi ya nyumbani kwa idadi ya watu inayokadiriwa kuwa asilimia 50. Ni chanzo muhimu cha madini na kuongeza nguvu mwilini, protini, madini ya chuma (iron) vitamini na madini mengine asilia.Waafrika hutumia mahindi kwa njia mbalimbali – (uji, ugali na pombe). Na mahindi ya kuchoma. Kila sehemu ya mmea wa mahindi ina thamani kiuchumi : punje, majani, shina na magunzi huweza kutoa kiasi kikubwa cha bidhaa nyinginezo zilizo chakula na zisizokuwa chakula.

KANUNI ZA KILIMO BORA CHA MAHINDI.

 
KANUNI YA KWANZA
Panda mapema
Tayarisha shamba mapema kwa zana yoyote iliyo ndani ya uwezo wako (jembe, maksai, trekta).
Kwa wilaya ya Mbozi Panda kuanzia tarehe 15 Novemba hadi kati kati ya mwezi Desemba.

Wednesday, October 29, 2014

Ugonjwa

Ugonjwa umezuka huko morogoro unaoenezwa kupitia maziwa yasiochemshwa vizuri na nyama ambazo hazijaiva vizuri